Yanga - Local

Yanga kuitikia mwaliko wa Rais Ikulu leo

Joel JJ By Joel JJ
5 Jun 2023
Yanga kuitikia mwaliko wa Rais Ikulu leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan leo Juni 05, 2023 ameialika timu ya Yanga kupata chakula cha jioni Ikulu, Dar es Salaam ikiwa ni pongezi kwa kufanya vizuri katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema timu nzima itahudhuria mwaliko huo kabla ya kuelekea mkoani Mbeya wanakokabiliwa na mechi mbili za ligi kuu dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Hersi amesema Yanga ilipaswa kuondoka Dar es salaam leo saa 1 usiku kuelekea Mbeya lakini sasa wataondoka baada ya kuhudhuria mwaliko wa Rais Samia ambaye pia ametoa ndege kuwapeleka mkoani Mbeya

Rais Samia amekuwa chachu ya mafanikio kwa klabu za Yanga na Simba msimu huu kwenye mashindano ya CAF akitoa bonus ya fedha kwa kila hatua ambayo kila timu ilifikia

Wakati Simba ilitolewa hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika, Yanga imefanikiwa kutinga fainali na kukosa ubingwa kwa mujibu wa kanuni tu baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya USM Alger

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
3h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
6h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
6h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
7h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
7h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
7h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
7h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
8h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →