Manchester City mabingwa Ulaya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th June 2023


Manchester City mabingwa Ulaya

Manchester City imetwaa taji la kwanza la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Inter Milan ya Italia usiku wa Jumamosi katika Uwanja wa Ataturk Olynmpiya huko Uturuki

Bao pekee la Manchester City lilifungwa na kiungo wa Kimataifa wa Hispania, Rodri dakika ya 68

Licha ya Manchester City kutawala kwa muda mwingi, ulikuwa mchezo wa nafasi chache Inter Milan wakiwa imara katika kujilinda

Kama sio umahiri wa mlinda lango wa Manchester City Ederson, Inter Milan wangeweza kurejesha bao hilo kwenye dakika za majeruhi Inter wakifanya mashambulizi makali langoni kwa Man City

Manchester City imefikia rekodi ya kushinda mataji matatu katika msimu mmoja, rekodi iliyowekwa na mahasimu wao Manchester United mwaka 1999

Linakuwa taji la kwanza kwa kocha Pep Guardiola kushinda tangu alipoondoka FC Barcelona, likiwa ni taji lake la tatu la Ligi ya Mabingwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.