Ni Azam Fc vs Yanga, fainali FA leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th June 2023


Ni Azam Fc vs Yanga, fainali FA leo

Leo msimu wa mashindano 2022/23 unahitimishwa mkoani Tanga kwa mchezo wa fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) kati ya Yanga dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa saa 9 Alasiri katika uwanja wa Mkwakwani

Baada ya mchezo huo usiku kutakuwa na tukio la utowaji tuzo kwa waliofanya vizuri Ligi Kuu, Ligi ya Wanawake na kombe la FA msimu wa 2022/23

Huu unaweza kuwa msimu bora zaidi kwa Yanga kama itaweza kutwaa kombe la FA na utakuwa msimu wa pili mfululizo kushinda taji hilo

Baada ya kutwaa Ngao ya Jamii, Ligi Kuu na kucheza fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC), Wananchi wana matarajio leo wanaweza kuongeza taji la tatu kabatini kama walivyofanya msimu uliopita

Hata hivyo wanakutana na Azam Fc ambayo ubingwa wa FA yatakuwa mafanikio yao makubwa zaidi kuyapata katika misimu ya hivi karibuni

Azam Fc walifika mapema jijini Tanga huku Kaimu Kocha Mkuu wa timu hiyo Kali Ongara akitamba kuwa wana kila sababu ya kushinda taji la FA leo

Yanga inashuka uwanjani leo bila ya mshambuliaji wake kinara wa mabao Fiston Mayele ambaye yuko kwenye majukumu ya timu ya Taifa sambamba na Stephane Aziz Ki


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.