Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Juni 14 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jun 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Juni 14 2023

Manchester United itaongoza kinyang'anyiro cha kumnunua fowadi wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, kutoka Paris St-Germain ikiwa klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza itanunuliwa na Sheikh Jassim bin Hamad Al Thani. (Metro)

Chelsea pia wanatarajiwa kumtaka Mbappe baada ya mshambuliaji huyo kuwaambia PSG kuwa hataki kuongeza mkataba wake nao zaidi ya 2024. (Times – Subscription Required).

Real Madrid pia wanataka kumsajili Mbappe msimu huu wa joto, jambo ambalo litaboresha uwezekano wa Tottenham kumbakisha mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 29, ambaye pia amekuwa akihusishwa na klabu hiyo ya Uhispania. (Mail)

Hata hivyo, wawakilishi wa Kane pia wamekutana na viongozi wa PSG. (Mirror)

Manchester United wako tayari kumuuza winga wa England Jadon Sancho, lakini wakati Aston Villa wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, hawataki kulipa bei inayotakiwa ya pauni milioni 60. (Football Transfers)

Arsenal hawana mpango wa kumrejesha tena mchezaji aliyevunja rekodi ya klabu kwa pauni milioni 72 Nicolas Pepe katika kikosi chao na wanataka kumuuza mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 28 msimu huu. (Telegraph – Subscription Required)

Mshambulizi wa Chelsea na Ubelgiji Romelu Lukaku, 30, amepewa ofa ya pauni milioni 20 kwa msimu na klabu ya Al-Hilal ya Saudi Arabia. (Guardian)

Aston Villa na Wolverhampton Wanderers wanavutiwa na kiungo wa kati wa Borussia Monchengladbach Mfaransa Manu Kone, 22, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Liverpool. (Mail)

Tottenham wanakaribia kuafikiana na kipa wa Brentford David Raya, 27, na wanatumai kujadili ada ya chini na The Bees, ambao wanataka pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania. (Standard)

Beki wa Barcelona na Uhispania Jordi Alba, 34, yuko kwenye mazungumzo na Inter Miami kuhusu kuhamia Ligi Kuu ya Soka. (Fabrizio Romano)

Barca wanamfuatilia kiungo wa kati wa Villarreal Mhispania Alex Baena, 21, kama mbadala wa kiungo wa kati wa Manchester City na Ujerumani Ilkay Gundogan, 32. (ESPN)

Coventry City wanavutiwa na beki wa Chelsea mwenye umri wa miaka 20 Muingereza Bashir Humphreys. (Standard)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’