Simba kuboresha benchi la ufundi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th June 2023


Simba kuboresha benchi la ufundi

Simba huenda ikamrejesha kocha wa magolikipa Milton Nienov ambaye amemaliza mkataba na Yanga

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Salim Abdallah 'Try Again' amebainisha kuwa wamefanya tathmini ya mambo yaliyowakwamisha kushinda taji lolote msimu huu

Uongozi wa Simba umedhamiria kufanya marekebisho katika usajili wa wachezaji pamoja na maboresho ya benchi la ufundi

Nienov alijiunga na Yanga baada ya Simba kusitisha mkataba wake sambamba na Kocha viungo Adel Zrane na Didie Gomez aliyekuwa kocha mkuu

Simba ilichukua uamuzi huo mwaka 2021 baada ya kutolewa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa na Jwaneng Galaxy

Aidha Simba pia inahusishwa na Kocha wa viungo kutoka klabu ya Rayon Sport Hategekimana Corneille

Corneille amewahi kufanya kazi na Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira wakati akiinoa Rayon msimu wa 2018/19


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.