Mmiliki wa Fountain Gate, Japhet Makau amenunua hisa zote za klabu ya Singida Big Stars hivyo ni rasmi anaimiliki timu hiyo kutoka Singida
Uongozi wa Singida BS umethibitisha timu hiyo kuuzwa katika Mkutano na Waandishi wa habari mapema leo
Singida Big Stars itabadili tena jina na kuitwa SINGIDA FOUNTAIN GATE FC na Makau anatarajiwa kuwa Rais na Mmiliki wa timu hiyo huku Makao Makuu ya timu yakiendelea kuwa mkoani Singida na dimba la Liti ndio Maskani yao
Kimuundo Makau atakuwa Rais na ataongoza Bodi yenye Wajumbe tisa



