Yanga - Local

Tutaleta kocha wa viwango - Kamwe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Jun 2023
Tutaleta kocha wa viwango - Kamwe

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema mchakato wa kusaka kocha mpya umeanza na tayari wamepokea CV nyingi za makocha

Kamwe amesema uongozi wa Yanga utaendesha mchakato wa kusaka kocha mpya kwa weledi na umakini ili kuhakikisha Kocha atakayekuja ataendeleza mazuri yalioachwa na Nasreddine Nabi

"Baada ya kutangaza kuondoka kwa kocha Nabi, katika saa 24 zilizopita tumepokea zaidi ya CV 1000 za makocha wanaotaka kuja kuifundisha timu yetu"

"Niwaambie wapenzi na wanachama wetu kuwa uongozi wao uko makini na wataleta kocha mwenye viwango ambaye ataweza kutimiza malengo ya klabu"

"Tunaheshimu uamuzi wa Kocha Nabi ambaye tulipenda kuendelea nae lakini ameona ni wakati sahihi kwake kwenda kutafuta changamoto mahali pengine baada ya mafanikio aliyotupa katika misimu miwili iliyopita," alisema Kamwe

Nabi anatarajiwa kujiunga na klabu ya Kaizer Chiefs baada ya misimu miwili na nusu na mafanikio katika klabu ya Yanga

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’