Stars karata muhimu dhidi ya Niger leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th June 2023


Stars karata muhimu dhidi ya Niger leo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inatupa karata muhimu uwanja wa Benjamin Mkapa ukiwa ni mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu michuano ya Afcon 2023 dhidi ya Niger

Tanzania inahitaji kushinda leo ili kuweka hai matumaini ya kufuzu huku ikiomba Uganda ipoteze mchezo dhidi ya Algeria ambao utapigwa huko Cameroon

Algeria tayari imefuzu wakati Tanzania, Uganda na Niger bado zinachuana kuwania nafasi ya pili

Tanzania inashika nafasi ya pili kundi F ikiwa na alama nne sawa na Uganda wakati Niger inashika nafasi ya nne ikiwa na alama mbili

Mechi ya mwisho kwa Tanzania ni ugenini dhidi ya Algeria hivyo kufanya mchezo wa leo dhidi ya Niger kuwa lazima kushinda na kwenda kusaka angalau alama moja huko Algeria

Mchezo utapigwa saa 10 jioni katika uwanja wa Benjamin Mkapa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.