Klabu ya Simba imethibitisha kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba wa kiungo mkabaji Victor Akpan raia wa Nigeria
Akpan alijiunga na Simba msimu uliopita akitokea klabu ya Coastal Union hata hivyo hakuweza kukidhi mahitaji ya Simba ambapo alitolewa kwa mkopo kwenda klabu ya Ihefu Fc
Taarifa iliyotolewa na Simba imebainisha kuwa Akpan hatakuwa sehemu ya kikosi cha wekundu hao wa Msimbazi msimu ujao
Akpan anakuwa mchezaji wa pili kuachwa na Simba baada ya Augustine Okrah
Wababe hao wa soka ukanda wa Afrika Mashariki na kati wana mkakati mzito wa maboresho ya kikosi



