Baada ya Azam Fc kuongoza kwa idadi ya wachezaji waliotangaza kuachana nao, klabu za Simba na Yanga nazo zinazidi kuongeza idadi
Jana klabu ya Simba ilitangaza kuachana na kiungo mshambuliaji Nelson Okwa baada ya makubaliano ya pande mbili kufikiwa
Okwa alikuwa mchezaji wa nne kuachwa na Simba baada ya Augustine Okrah, Victor Akpan na Mohammed Ouattara
Usiku Yanga nayo ikatangaza kuachana na winga mtukutu Bernard Morrison ambaye mkataba wake wa mwaka mmoja na Yanga umemalizika
Morrison alikuwa mchezaji wa tatu kuachwa na Yanga baada ya Dickson Ambundo na Tuisila Kisinda



