Ligi ya Thank You inaendelea Simba, Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd June 2023


Ligi ya Thank You inaendelea Simba, Yanga

Baada ya Azam Fc kuongoza kwa idadi ya wachezaji waliotangaza kuachana nao, klabu za Simba na Yanga nazo zinazidi kuongeza idadi

Jana klabu ya Simba ilitangaza kuachana na kiungo mshambuliaji Nelson Okwa baada ya makubaliano ya pande mbili kufikiwa

Okwa alikuwa mchezaji wa nne kuachwa na Simba baada ya Augustine Okrah, Victor Akpan na Mohammed Ouattara

Usiku Yanga nayo ikatangaza kuachana na winga mtukutu Bernard Morrison ambaye mkataba wake wa mwaka mmoja na Yanga umemalizika

Morrison alikuwa mchezaji wa tatu kuachwa na Yanga baada ya Dickson Ambundo na Tuisila Kisinda


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.