Yanga - Local

Yanga kuanza na Kocha Mkuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jun 2023
Yanga kuanza na Kocha Mkuu

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema klabu hiyo itamtangaza Kocha wake Mkuu baada ya Mkutano Mkuu wa Wanachama ambao utafanyika Jumamosi, Juni 24 jijini Dar es salaam

Kamwe amesema kocha atahusika na michakato yote ya usajili, hivyo baada ya kutambulishwa atafanya kazi na viongozi katika usajili

Aidha Kamwe amebainisha kuwa hatma ya kocha msaidizi Cedric Kaze na wengine katika benchi la ufundi itategemea na mapendekezo ya kocha wao mpya

"Baada ya Mkutano Mkuu tutamtangaza Kocha Mkuu, kisha tutaanza kutangaza Wachezaji wapya. Sisi sio kama zile klabu zingine, tutatambulisha kocha kisha Wachezaji ili aijenge timu yeye mwenyewe"

"Kuhusu Cedric Kaze, tutamuuliza kocha mpya, kama atakuwa na wasaidizi wake basi Cedric Kaze tutampangia kazi nyingine," alisema Kamwe

Kamwe pia amethibitisha klabu ya Yanga kuanza mazungumzo ya kumuongeza mkataba mshambuliaji wao kinara, Fiston Mayele

"Kwanza ieleweke, Mayele ni mchezaji wa Yanga ana mkataba wa mwaka mmoja, mazungumzo yakuboresha mkataba ni jambo la kawaida kwa klabu yetu pale mchezaji anapofanya vizuri"

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’