Klabu ya Simba imeanza mazungumzo ya kumsajili winga wake wa zamani Luis Miquissone kulingana na Mwanahabari raia wa Ghana, Micky Junior
Mabosi wa Simba wamefanya mazungumzo ya awali na Al Ahly ambapo mabingwa hao wa kihistoria ligi ya mabingwa wamebainisha kuwa Miquissone yuko sokoni
Simba iko tayari kumsajili kwa mkopo, changamoto ikiwa bado kwenye mshahara ambapo Al Ahly hawako tayari kulipa mshahara wa mchezaji huyo kama anatoka kwa mkopo kwani lengo lao ni kumuuza
Wakati huohuo Simba ikiwa tayari kulipa asilimia 30 ya mshahara wa Miquissone ambao unatajwa kuwa Tsh Milioni 93
Aidha kwa upande wa Miquissone mwenyewe ametoa masharti kuwa hayuko tayari kupunguza mshahara wake kama atatolewa kwa mkopo
Miquissone na Walter Bwalya hawako kwenye mipango ya Al Ahly msimu ujao na hivyo wote watauzwa na timu hiyo