Baada ya kuonyesha kiwango bora tangu ujio wa kocha Robertinho Oliveira, mshambuliaji Kibu Denis yuko katika mazungumzo na uongozi wa Simba ili kuongeza mkataba
Kibu ni miongoni mwa wachezaji ambao Robertinho alipendekeza wapewe mikataba mipya baada ya mkataba wake wa awali uliokuwa wa miaka miwili kumalizika
Kibu alimaliza msimu 'kibabe' akiwa miongoni mwa wachezaji bora katika kikosi cha Simba
Mara kadhaa Robertinho alieleza kuvutiwa na uchezaji wake akibainisha kuwa mchezaji huyo anajituma sana katika mechi na hata anapokuwa mazoezini
Jitihada zake zimemrejesha kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars