Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amesema kuwa mechi za Ngao ya Jamii zitapigwa uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga
Karia amesema kwa mara ya kwanza katika Ngao ya Jamii zitachezwa mechi tatu, mbili za nusu fainali na moja ya fainali
Karia amesema uwanja wa Mkwakwani utatumika kwa kuwa uwanja wa Benjamin Mkapa utakuwa bado umefungwa ukikarabatiwa
Timu nne zitashiriki Ngao ya Jamii ambazo ni Yanga, Simba, Azam Fc na Singida Fountain Gate Fc