Ni rasmi klabu ya Simba imetangaza kuwa kambi ya maandalizi ya msimu mpya 2023/24 ni nchini Uturuki
Taarifa iliyotolewa na Simba, imebainisha kuwa nyota wote ikiwa ni pamoja na wale waliosajiliwa katika dirisha hili, watajumuishwa katika safari hiyo
Ikiwa Uturuki Simba itacheza mechi tatu za kirafiki, wekundu hao wa Msimbazi wakitarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa mwezi huu
Leo Simba imeanza kuwafanyia wachezaji vipimo vya afya tayari kwa maandalizi hayo ya 2023/24



