Geita Gold yaacha saba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th July 2023


Geita Gold yaacha saba

Afisa Mtendaji Mkuu wa Geita Gold Fc Simon Shija amesema timu hiyo inatarajiwa kufanya maboresho makubwa katika dirisha hili ya usajili

Geita Gold ilimaliza nafasi ya saba katika msimamo wa ligi 2022/23 timu hiyo ikiwa imeshuka kwa nafasi tatu kutoka nafasi ya nne waliyomaliza msimu wa 2021/22

Shija amesema mpaka sasa wamewakabidhi wachezaji saba barua za kuachana nao lakini pia wapo wengine wataachwa

"Kwa sasa tumewapa barua wachezaji saba lakini wengine watatu bado tunaendelea kuongea nao tena na kama tutashindwana basi nao tutawafungulia mlango wa kutokea japo hatutamani hilo kutokea"

Shija aliongeza moja ya mchezaji waliopo kwenye mazungumzo ya mkataba mpya ni Elias Maguri ambaye wanatamani kuendelea naye msimu ujao baada ya kuonyesha kiwango kizuri tangu ajiunge nao

Wachezaji waliopewa ‘Thank You’ ni; Fabrice Kayemba, Arakaza MacArthur, Shown Oduro, Mussa Gadi, Jeremiah Thomas na mchezaji raia wa Japan


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.