Klabu ya Azam Fc imemtambulisha Khalifa Ababakar Fall kuwa kocha wa makipa na Ibrahim Diop kuwa mchambuzi wa mechi (Video Analyst)
Wataalam hao wote ni raia wa Senegal, walitangazwa kutua Azam Fc siku ya Jumatatu
Azam Fc inanolewa na Youssouph Dabo ambaye alikabidhiwa mikoba mwishoni mwa msimu uliopita akichukua nafasi ya Kali Ongala ambaye aliondoka baada ya msimu kumalizika
Matajiri hao wa Chamazi wameanza maandalizi ya pre-season ambapo wameanza kwa zoezi la kuwafanyia wachezaji vipimo vya afya



