Klabu ya Yanga imetangaza usajili wa kiungo mshambuliaji Nickson Kibabage kutoka klabu ya Singida Fountain Gate
Kibabage ambaye pia anamudu kucheza nafasi ya beki wa kushoto na winga, amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Yanga
Nyota huyo aliyewahi kuzitumikia Difaa El Jadid (Morocco), KMC na Mtibwa Sugar, atajumuishwa katika kikosi cha Yanga kitakachosafiri kwenda Malawi kwa ajili ya mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Nyasa Big Bullets Julai 06 katika maadhimisho ya sherehe za Uhuru wa Malawi
Ndiye mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Yanga katika dirisha hili la usajili lililofunguliwa Julai 01