Klabu ya Simba imetangaza usajili wa Kiungo Mshambuliaji kutoka klabu ya Rayon Sports ya nchini Rwanda, Leandre Willy Onana
Onana raia wa Cameroon, ametua Msimbazi kwa mkataba wa miaka miwili
Onana ametua Simba huku akiacha kumbukumbu nchini Rwanda ya kuwa Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya nchini humo msimu huu 2022/23, akifunga mabao 16 na sasa anatarajiwa kuendeleza kasi hiyo ya kufunga na kutengeneza mabao Msimbazi
Onana ni miongoni mwa wachezaji ambao tayari wamefanyiwa vipimo vya afya na Simba kuelekea pre-season itakayofanyika Uturuki



