Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Julai 10 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Julai 10 2023

Juventus wameiambia Chelsea kuwa wanaweza kumpata mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 23, kwa kutoa euro 25m (£21.4m) pamoja na mshambuliaji wao wa Ubelgiji Romelu Lukaku. (Corriere dello Sport, via Football London)

Hata hivyo, Lukaku, 30, yuko tayari kukatwa mshahara wa £1m kwa mwaka ili kurejea kwa mkataba wa kudumu Inter Milan baada ya muda wake wa mkopo kumalizika.(Telegraph)

Chelsea wameiambia Inter kuhusu Juventus kutaka kumnunua Lukaku ili kujaribu kuongeza bei, jambo ambalo limewakasirisha Juve. (Tuttosport, via Mirror)

Bayern Munich wametoa ofa iliyoboreshwa zaidi ya £70m kwa mshambuliaji wa Tottenham na Uingereza Harry Kane, 29. (Guardian)

Meneja mpya wa Al-Ettifaq Steven Gerrard amefanya mazungumzo na winga wa Ivory Coast Wilfried Zaha kuhusu uhamisho wa £16m kwa mwaka kwenda Saudi Arabia, huku kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 na Crystal Palace sasa ikimalizika. (Mail)

Manchester United wanajiandaa kuwasilisha ofa mpya kwa Atalanta kwa ajili ya Rasmus Hojlund, wakiwa tayari wameafikiana kimsingi na mshambuliaji huyo wa Denmark, 20, kuhusu mkataba wa miaka mitano hadi 2028. (Nicolo Schira).

Fulham na Crystal Palace wana nia ya kumsajili beki wa pembeni wa Marekani Sergino Dest, 22, kutoka Barcelona. (Mundo Deportivo)

Wolfsburg wako tayari kumbakisha Micky van de Ven ikiwa Tottenham hawatakidhi bei yao ya £40m kumnunua mlinzi huyo wa Uholanzi, 22. (Wolfsburger Allgemeine, via Express)

Winga wa Leicester Muingereza Harvey Barnes, 25, anataka kuhamia Newcastle msimu huu wa joto. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Fred, 30, amebadilisha wakala wake huku klabu za Fulham na Saudi Arabia zikiwa na nia ya kutaka kumsajili (Fabrizio Romano)

Paris St-Germain wanaweza kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, kama mbadala wa mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24. (Gazzetta dello Sport, via Football Italia)

Gwiji wa zamani wa Marekani Landon Donovan amemkosoa winga wa Chelsea Mmarekani Christian Pulisic, 24, kwa kuchagua kujiunga na AC Milan badala ya kuhamia ligi ya Marekani, MLS. (Fox Sports)

Mkufunzi wa Roma Jose Mourinho anatamani kumsajili kiungo wa kati wa Scotland Scott McTominay, 26, kutoka klabu yake ya zamani ya Manchester United. (Football transfers)

Manchester United na Newcastle zote zinataka kumnunua mlinzi wa Ufaransa Axel Disasi, 25, lakini hakuna timu iliyowasilisha ofa rasmi kwenda Monaco. (Fabrizio Romano)

Beki wa Uholanzi Jurrien Timber, 22, amefanyiwa vipimo vya afya na Arsenal na kurejea nyumbani kwa ajili ya kuaga wenzie kabla ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Ajax. (Metro)

Everton wametuma ofa kwa beki wa zamani wa Uingereza Ashley Young, 38, baada ya mkataba wake kumalizika pale Aston Villa. (Football Insider)

Liverpool wako tayari kumruhusu mlinzi wa Uingereza Nat Phillips, 26, kujiunga na Leeds - lakini kwa mkataba wa kudumu pekee. (Sun)

Manchester United itasikiliza ofa za mkopo kwa ajili ya winga wa Ivory Coast Amad Diallo, 20, ambaye alitumia msimu uliopita kucheza kwa mkopo Sunderland. (Football Insider)

West Ham wameonyesha nia yao ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Senegal Habib Diallo, 28, kutoka Strasbourg. (Football Insider)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.