Simba kutimkia Uturuki Jumanne

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th July 2023


Simba kutimkia Uturuki Jumanne

Kikosi cha Simba kinaondoka nchini kesho Jumanne Julai 11 kuelekea Uturuki kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu mpya (2023/24)

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema Simba itaondoka nchini ikiwa na wachezaji wake wote waliosajiliwa katika dirisha hili na wale wengine wanaoendelea kikosini kutoka msimu uliopita

Ahmed amebainisha kuwa Simba itaweka kambi ya wiki tatu huko Uturuki kwa ajili ya pre-season na itarejea nchini August 01

"Tutaweka kambi ya wiki tatu hadi August 01 tutarejea nchini kwa ajili ya maandalizi ya Simba Day. Tukiwa Uturuki tunatarajiwa kucheza mechi tatu zakujipima nguvu dhidi ya timu za huko Ulaya"

"Kocha Robertinho tayari amewasili na benchi lake lote la ufundi pia wote wapo tayari kwa safari," alisema Ahmed

Ahmed amebainisha kuwa bado Simba haijakamilisha utambulisho wa wachezaji, wengine watatambulishwa wakati wowote kabla ya timu kuondoka hapo kesho


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.