Klabu ya Yanga imemtangaza mshambuliaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Senegal Moussa Ndao kuwa Kocha Msaidizi wa mabingwa hao wa Tanzania Bara
Ndao anachukua nafasi ya Cedric Kaze ambaye mkataba wake umemalizika
Ndao ambaye amewahi kucheza na kufundisha klabu ya Wydad Athletic, ni pendekezo la Kocha Miguel Gamondi
Klabu ya Yanga imemshukuru na kumtakia kila la kheri Kaze ambaye amekuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kilichoshinda mataji saba katika misimu miwili



