Mrithi wa Kaze Yanga ni huyu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th July 2023


Mrithi wa Kaze Yanga ni huyu

Klabu ya Yanga imemtangaza mshambuliaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Senegal Moussa Ndao kuwa Kocha Msaidizi wa mabingwa hao wa Tanzania Bara

Ndao anachukua nafasi ya Cedric Kaze ambaye mkataba wake umemalizika 

Ndao ambaye amewahi kucheza na kufundisha klabu ya Wydad Athletic, ni pendekezo la Kocha Miguel Gamondi

Klabu ya Yanga imemshukuru na kumtakia kila la kheri Kaze ambaye amekuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kilichoshinda mataji saba katika misimu miwili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.