Baada ya kuwasili Mji wa Ankara jana majira ya saa 1 usiku, wachezaji wa Simba walipata muda wa kupumzika na leo wanaanza rasmi program ya maandalizi ya pre-season
Meneja wa Simba Mikael Igendia amesema wamekuwa na safari nzuri kutoka jijini Dar es salaam mpaka Oman kisha kuunganisha ndege nyingine kutoka Oman mpaka Istanbul ambako pia walisafiri kuelekea Mji wa Ankara
Igendia amesema wachezaji na benchi la ufundi wako kamili na leo wanaanza rasmi mazoezi
Kundi la kwanza ambalo linaanza mazoezi huko Uturuki linajumuisha wachezaji 17 ambapo kundi la pili la wachezaji na baadhi ya viongozi wanatarajiwa kuondoka nchini siku ya Jumamosi
Simba itakuwa Uturuki hadi August 01 itakaporejea nchini tayari kwa SIMBA DAY