Simba yazima tetesi kuhusu Chama

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th July 2023


Simba yazima tetesi kuhusu Chama

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally 'amewakata maini' wale wanaodhani Simba ina mpango wa kuachana na kiungo wake kinara wa pasi za mwisho Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka'

Ahmed amesema Chama ambaye bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Simba yuko kwenye mipango ya Wekundu hao wa Msimbazi wala hakuna ofa iliyowasilishwa mezani kumtaka

Ahmed amewataka Wanasimba wapuuze taarifa zinazosambazwa huko kwenye mitandao ya kijamii kuhusu Chama kwani yupo sana

"Iko hivi, Chama bado ana mkataba na Simba kwa muda wa mwaka mmoja hadi Juni 30 2024. Hatujapokea ofa kutoka klabu yeyote ikihitaji kumnunua Chama na wala hatujapokea maombi ya mchezaji kutaka kuvunja mkataba"

"Mchezaji yeyote ambae tunamhitaji atabaki kuitumikia Simba kulingana na mahitaji ya mkataba wetu," alisema Ahmed

Chama anatarajiwa kuungana na wenzake katika pre-season huko Uturuki ambapo Ahmed amesema msafara wa pili utawasili Uturuki Jumatatu ukijumuishwa wachezaji wote waliobaki jijini Dar es salaam kutokana na sababu mbalimbali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.