Wakati wachezaji wa Simba waliokuwa wamebaki jijini Dar es salaam wakisafiri leo kuelekea Uturuki kuungana na wenzao kwa ajili ya pre-season, kiungo Clatous Chama ameendelea kubaki jijini Dar es salaam
Taarifa iliyotolewa na Simba mapema leo imebaninisha kuwa wachezaji Willy Onana, Jean Baleke na Che Fondoh Malone wamesafiri leo kuelekea Uturuki huku winga Aubin Kramo akitarajiwa kutua Uturuki leo akitokea Ivory Coast
Kiungo Fabrice Ngomba atasafiri baada ya kukamilisha vibali, sintofahamu imebaki kwa Chama ambaye zipo taarifa kuwa ameuambia uongozi wa timu hiyo amepata ofa nje ya nchi
Upo mgogogo wa kimkataba kati ya Chama na Simba ambapo nyota huyo anadai mkataba wake na wekundu hao wa Simba umemalizika huku uongozi wa Simba ukisisitiza bado mwaka mmoja
Taarifa za ndani zimebainisha kuwa viongozi wa Simba na Chama watakutana katika kikao kingine siku ya Jumanne ili kumaliza sintofahamu iliyojitokeza na pengine Chama huenda akasafiri kwenda Uturuki siku ya Alhamisi



