Nahodha wa timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) Mbwana Samatta amejiunga na klabu ya PAOK ya Ugiriki akitokea klabu ya Fenerbahce aliyovunja nayo mkataba
Samatta aliyekipiga KRC Genk msimu uliopita akiwa kwa mkopo akitokea Fernabache amejiunga na PAOK ambao msimu ujao watashiriki mashindano ya Ligi ya Europa
PAOK wameweka taarifa ya Samatta kujiunga na timu yao, lakini hawajaandika amejiunga na mkataba wa muda gani
Hii ni nafasi nyingine kwa Samatta kushiriki michuano ya Europa akipata mafanikio makubwa katika michuano hiyo misimu miwili iliyopita akiwa na KRC Genk na kupata nafasi ya kusajiliwa na Aston Villa ya Uingereza



