Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Julai 18 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Julai 18 2023

Mshambulizi wa Tottenham Harry Kane hana mpango kujiunga na Paris St-Germain msimu huu wa joto na mchezaji huyo wa miaka 29, ambaye anaaminika kuwa tayari kuhamia Bayern Munich, hatakubali mbinu yoyote kutoka kwa mabingwa hao wa Ufaransa. (Telegraph - usajili unahitajika)

Tottenham huenda wakamnunua mshambuliaji wa Brentford Ivan Toney, 27, ambaye anatumikia marufuku ya kutojihusisha na soka hadi Januari, ikiwa mchezaji mwenzake wa kimataifa wa Uingereza Kane ataondoka katika klabu hiyo. (Football Transfers)

Rais wa PSG Nasser Al-Khelaifi atakutana ana kwa ana na mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe kwa mara ya kwanza tangu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kutuma barua kwa klabu hiyo akisema hataongeza mkataba wake nao hadi mwisho wa msimu ujao. (Sky Sports)

Chelsea wanatarajiwa kuwasilisha dau lililoboreshwa la zaidi ya pauni milioni 70 kumnunua kiungo wa Brighton Moises Caicedo wiki hii, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ecuador mwenye umri wa miaka 21 akiwa tayari ameshakubaliana na The Blues. (Standard)

Mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 25, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na Manchester United ambao unatarajiwa kuendelea hadi 2028 na kuwa na thamani ya £325,000 kwa wiki. (Times - usajili unahitajika) West Ham wameungana na Manchester United kumsaka kiungo wa kati wa Bayern Munich na Ujerumani Leon Goretzka, 28. (Sky Germany)

Inter Milan wanatarajiwa kutoa ofa ya pauni milioni 34.3 kwa mshambuliaji wa Marekani Folarin Balogun wakati wakitafuta dili la mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, ambaye thamani ya Arsenal ni £50m. (Athletic -Usajili unahitajika)

Brighton wanaongoza Burnley na Leicester City katika kinyang'anyiro cha kumnunua kwa mkopo mshambuliaji wa England wa chini ya miaka-21 Cole Palmer kutoka Manchester City. (Telegraph - usajili unahitajika)

Brighton wako tayari kuipiku Fulham katika usajili wa beki wa Fiorentina Mbrazil Igor, 25. (Standard) Burnley na Leicester, pamoja na Sheffield United, wana hamu ya kumnunua kwa mkopo winga wa Manchester United na Ivory Coast Amad Diallo, 21 . (Mail)

Wolverhampton Wanderers wanajadiliana kuhusu usajili wa beki wa kimataifa wa Uswizi Nico Elvedi, 26, kutoka klabu ya Ujerumani Borussia Monchengladbach. (Express & Star)

Leeds United wamefikia mkataba na Chelsea kumsajili beki wa Wales Ethan Ampadu, 22, kwa £7m pamoja na nyongeza. (Usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.