Simba - Local - Transfer

Simba kukamilisha usajili wa golikipa

Joel JJ By Joel JJ
18 Jul 2023
Simba kukamilisha usajili wa golikipa

Katika wiki hii Simba inatarajiwa kufunga hesabu za usajili kwa kumtambulisha mlinda lango ambaye anatua kusaidiana na Ali Salim wakati Aishi Manula akiendelea kuuguza majeraha

Manula atarejea uwanjani katikati ya mwezi Oktoba pale atakapokuwa amepona majeraha baada ya kufanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Awali Simba ilikaribia kumsajili mlinda lango kutoka Brazil Caique Luiz Santos hata hivyo ilisitisha mpango huo baada ya kubaini golikipa huyo anafahanmu lugha moja tu, Kireno

Ni wazi angekabiliwa na changamoto katika kuwasiliana na wenzake hasa ikizingatiwa katika ukanda wetu lugha ya kireno sio miongoni mwa lugha zinazozungumzwa na wengi

Simba inatajwa kumuwania mlinda lango raia wa Cameroon Simon Omossola kutoka Fc Lupopo

Omosolla mwenye umri wa miaka 25 pia amewahi kuitumikia klabu ya AS Vita ya DR Congo hivyo ni mlinda lango ambaye ana uzoefu mkubwa katika mashindano ya CAF

Viongozi wa Simba wako kwenye presha kubwa ya kuhakikisha wanakamilisha dili la golikipa haraka ili apate nafasi ya kushiriki pre-season na wenzake huko Uturuki

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
4h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
7h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
7h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
8h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
8h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
8h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
8h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →