Simba kukamilisha usajili wa golikipa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th July 2023


Simba kukamilisha usajili wa golikipa

Katika wiki hii Simba inatarajiwa kufunga hesabu za usajili kwa kumtambulisha mlinda lango ambaye anatua kusaidiana na Ali Salim wakati Aishi Manula akiendelea kuuguza majeraha

Manula atarejea uwanjani katikati ya mwezi Oktoba pale atakapokuwa amepona majeraha baada ya kufanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Awali Simba ilikaribia kumsajili mlinda lango kutoka Brazil Caique Luiz Santos hata hivyo ilisitisha mpango huo baada ya kubaini golikipa huyo anafahanmu lugha moja tu, Kireno

Ni wazi angekabiliwa na changamoto katika kuwasiliana na wenzake hasa ikizingatiwa katika ukanda wetu lugha ya kireno sio miongoni mwa lugha zinazozungumzwa na wengi

Simba inatajwa kumuwania mlinda lango raia wa Cameroon Simon Omossola kutoka Fc Lupopo

Omosolla mwenye umri wa miaka 25 pia amewahi kuitumikia klabu ya AS Vita ya DR Congo hivyo ni mlinda lango ambaye ana uzoefu mkubwa katika mashindano ya CAF

Viongozi wa Simba wako kwenye presha kubwa ya kuhakikisha wanakamilisha dili la golikipa haraka ili apate nafasi ya kushiriki pre-season na wenzake huko Uturuki


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.