Chelsea wanafanyia kazi ofa iliyoboreshwa ya pauni milioni 80 pamoja na nyongeza kwa kiungo wa Brighton na Ecuador Moises Caicedo, 21. (Mail)
Chelsea pia wanafikiria kumrejesha Marc Guehi, miaka miwili baada ya kumuuza beki huyo wa Uingereza, 23, kwa Crystal Palace. (Guardian)
Manchester City wanamtaka winga wa Barcelona wa Brazil Raphinha, 26, kuchukua nafasi ya winga wao anayekwenda Al-Ahli kutoka Algeria Riyad Mahrez, 32. (Foot Mercato - kwa Kifaransa)
Newcastle wanakaribia kumuuza winga Mfaransa Allan Saint-Maximin, 26, kwa klabu ya Saudi Arabia Al-Ahli kwa takriban pauni milioni 30. (Telegraph - usajili unahitajika)
Al-Nassr wameboresha dau lao la kumnunua Moussa Diaby wa Bayer Leverkusen, huku Aston Villa wakiwasilisha ombi la pili kwa winga huyo wa Ufaransa, 24. (Fabrizio Romano).
Crystal Palace inatarajiwa kuweka thamani ya kima cha chini cha pauni milioni 70 kwa kiungo wa kati wa Mali Cheick Doucoure, 23, ambaye ananyatiwa na Liverpool. (Mail)
ottenham wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Brazil Pedro, 26, anayechezea Flamengo. (Independent)
Dau la pauni milioni 15 linaweza kutosha kwa Bournemouth kushinda vilabu vya Borussia Dortmund, Barcelona na Real Madrid katika usajili wa beki wa Uhispania Ivan Fresneda, 18, kutoka Real Valladolid msimu huu. (Football Insider)
Fulham wametoa ofa ya awali ya £15m kwa Ajax kumnunua beki wa Nigeria Calvin Bassey, 23. (Athletic -Usajili unahitajika)
Mshambulizi wa Serbia Aleksandar Mitrovic, 28, amesema hatawahi kuichezea Fulham tena baada ya kukataa ofa mbili kutoka kwa Al-Hilal. (Sky Sports)
Atletico Madrid wamempa mshambuliaji wa Ureno Joao Felix, 23, idhini ya kukamilisha uhamisho wake kwenda Barcelona. (AS - kwa Kihispania)
Atletico wamewasiliana na Paris St-Germain kuhusu upatikanaji wa Marco Verratti lakini bado hawajatuma ofa kwa kiungo huyo wa kati wa Italia, 30. (L'Equipe - kwa Kifaransa)
Chelsea huenda wakakamilisha uhamisho wa Elye Wahi wa Montpellier lakini Atletico Madrid pia wanamwania mshambuliaji huyo wa Ufaransa, 20. (L'Equipe - in French)
Tottenham wameungana na West Ham katika kinyang'anyiro cha kumnunua Conor Gallagher msimu huu wa joto kutoka Chelsea, ambao wanaaminika kushikilia ada ya angalau £40m kwa kiungo huyo wa kati wa Uingereza, 23. (Football Insider)
Arsenal wanamfuatilia kiungo wa Dinamo Zagreb Martin Baturina, 20, ambaye aliivutia Croatia kwenye michuano ya Uropa ya Vijana chini ya miaka 21. (Express)
Villarreal wana nia ya kumsajili beki wa Ureno Cedric Soares, 31, kutoka Arsenal. (Sport - kwa Kihispania)
Real Betis wanavutiwa na kiungo wa kati wa West Ham na Uhispania Pablo Fornals, 27, pamoja na kiungo wa kati wa Tottenham na Argentina Giovani lo Celso, 27. (Relevo - kwa Kihispania)
Tottenham wamempa beki wa Colombia Davinson Sanchez, 27, ruhusa ya kufanya mazungumzo na Strasbourg na Spartak Moscow. (Dakika 90)
Wolves wako kwenye mazungumzo ya kumsajili beki wa zamani wa Uingereza Aaron Cresswell, 33, kutoka West Ham. ( Athletic -Usajili unahitajika)
Napoli na Torino wako mbioni kumsajili kiungo wa kati Mfaransa Boubakary Soumare, 24, kutoka Leicester. (L'Equipe - kwa Kifaransa)
BBC



