Klabu ya Simba jana ilitambulisha usajili wa wachezaji watatu wa ndani ambao wamefunga usajili kwa wachezaji wa ndani
Mshambuliaji Shabani Iddi Chilunda, kiungo Abdallah Khamis na beki Hussein Kazi walitambulishwa kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi
Chilunda ametua Simba akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba na Azam Fc wakati Khamis amejiunga na Simba akitikeo klabu ya Tusker Fc ya Kenya
Kazi ametua Msimbazi akitokea klabu ya Geita Gold
Bado Simba imebakisha utambulisho wa wachezaji wengine wawili wa kigeni mmoja akiwa ni mlinda lango na pili ni Luis Miquissone



