Skudu awaalika mashabiki Wiki ya Mwananchi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st July 2023


Skudu awaalika mashabiki Wiki ya Mwananchi

Winga wa Yanga Mahlatse Makudubela 'Skudu' amewaalika mashabiki wa soka nchini kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kushuhudia mtanange wa kilele cha wiki ya Mwananchi dhidi ya Kaizer Chiefs ambao utapigwa kesho Jumamosi

Akizungumza katika mkutano na Wanahabari kuelekea mchezo huo, Skudu amesema wamewaandalia mashabiki burudani kubwa wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa

"Tupo kwenye maandalizi ya awali kujiandaa na msimu mpya, kwa niaba ya wachezaji wenzangu kwanza niseme ni heshima kubwa sana kwangu kuwaalilisha kwenye mkutano huu na ujumbe wetu kwenu tunaomba kesho mje kwa wingi tumewaandalia burudani nzuri," alisema

Skudu ndiye mchezaji aliyekabidhiwa jezi namba sita ambayo kwa takribani mwezi mmoja ilinadiwa na viongozi wa Yanga

Amesema kukabidhiwa jezi hiyo ni heshima kubwa kwake, na atahakikisha anailinda thamani yake


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.