Ulimwengu kuibukia Singida FG

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd July 2023


Ulimwengu kuibukia Singida FG

Klabu ya Singida FG iko mbioni kukamilisha usajili wa mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye alikuwa anacheza kikosi cha TP Mazembe. Ulimwengu kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Mazembe

Ulimwengu na mastaa wengine ambao hawajatambulishwa tayari wapo kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea mkoani Arusha kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya

Kama Ulimwengu atasaini mkataba wa kuitumikia timu hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kucheza soka nchini

Upande wa Singida ni wazi usajili wa Ulimwengu unaenda kuongeza kitu katika kikosi chao kwani mchezaji huyo akiwa fiti anakuwa na ubora mzuri wa kuweka mipira wavuni

Ulimwengu ana uzoefu wa mashindano makubwa kwani alishachukua ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2014/15 na alicheza Fainali za kombe la Dunia upande wa klabu 2016 akiwa na TP Mazembe


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.