Klabu ya Singida FG iko mbioni kukamilisha usajili wa mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye alikuwa anacheza kikosi cha TP Mazembe. Ulimwengu kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Mazembe
Ulimwengu na mastaa wengine ambao hawajatambulishwa tayari wapo kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea mkoani Arusha kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya
Kama Ulimwengu atasaini mkataba wa kuitumikia timu hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kucheza soka nchini
Upande wa Singida ni wazi usajili wa Ulimwengu unaenda kuongeza kitu katika kikosi chao kwani mchezaji huyo akiwa fiti anakuwa na ubora mzuri wa kuweka mipira wavuni
Ulimwengu ana uzoefu wa mashindano makubwa kwani alishachukua ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2014/15 na alicheza Fainali za kombe la Dunia upande wa klabu 2016 akiwa na TP Mazembe



