Yanga - Local

Nyota wapya Yanga wapagawisha mashabiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jul 2023
Nyota wapya Yanga wapagawisha mashabiki

Jana Yanga ilicheza mechi ya kuhitimisha kilele cha wiki ya Mwananchi dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini

Mchezo huo wa Kimataifa wa kirafiki ulipigwa uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 1 usiku Yanga ikiibuka na ushindi wa bao 1-0

Mfungaji wa bao pekee la Yanga alikuwa ni Kennedy Musonda akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Max Nzengeli

Furaha ya mashabiki wa Yanga ni kuwashuhudia nyota wao wapya wakiwa katika kiwango bora

Kulikuwa na maneno mengi katika dirisha hili la usajili kila timu ikitamba kufanya usajili mzuri, nyota waliosajiliwa na Yanga wamedhihirisha ubora wao katika siku ya kwanza kazini

Nickson Kibabage, Jonas Mkude, Max, Skudu Makudubela, Yao Yao, Gift Fred wote wakipata nafasi ya kucheza dakika 45

Mkude aliwapagawisha mashabiki wa Yanga kwa uwezo wake wa kupiga pasi ndefu wakati Max anaweza kuwa shujaa mpya katika kikosi cha Yanga kutokana na umahiri wake anapokuwa na mpira mguuni

Kibabage alionyesha umahiri pale timu inaposhambulia akishirikiana vyema na Skudu

Kwa hakika ulikuwa mchezo mzuri ambao umewapa picha mashabiki wa Yanga nini watarajie kutoka kwa timu yao

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
8h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
9h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’