Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema mchezo dhidi ya Kaizer Chiefs umempa taswira nzuri ya aina ya kikosi alichonacho
Aidha Gamondi ameeleza kuridhishwa na ari, morali na upambanaji wa wachezaji wake huku akiwamwagia sifa kwa kuonyesha kiwango kizuri
"Wanapongeza wachezaji wangu kwa kuwa na mchezo mzuri leo. Tulitawala mchezo na tulitengeneza nafasi nyingi pengine tungeweza kufunga mabao zaidi"
"Nikuhakikishie tuna wachezaji bora na zaidi wako wengine wamenishtua kwa viwango vyao, tuna timu ya kuendelea kuipigania Yanga kupata mataji zaidi"
"Nimewaambia wachezaji tunachotakiwa ni kujiandaa timu ishinde kila mechi ndio maana tupo hapa na hatua hiyo inaanzia sasa hadi mwisho wa msimu, mashabiki wetu wanahitaji kutuona tunavuja jasho jingi kwa ajili ya timu hii kubwa," alisema Gamondi
Gamondi amekiandaa kikosi chake kwa takribani siki moja tu kabla ya mchezo huo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0
Jambo lililowafurashisha mashabiki wa Yanga ni kuona aina ya uchezaji wa timu yao haujabadilika zaidi yapo maboresho yameongezeka hasa timu inapokwenda kushambulia, kasi inaongezeka



