Klabu ya Simba imetangaza Wiki ya Simba itakayoanza Julai 29 ambayo kilele chake ni August 06 pale uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo kutakuwa na burudani zitakazohitimishwa na mchezo wa Kimataifa wa kirafiki
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed ametangaza kauli mbiu ya Simba Day ya mwaka huu ni UNYAMA MWINGI
Ahmed amesema Wiki ya Simba itazinduliwa rasmi Agosti Mosi eneo la Buza Kanisani wilayani Temeke ambapo atakuwepo na kispika chake ambacho amekuwa akitumia katika hamasa za kuwaita mashabiki uwanjani.
Katika wiki ya Simba kutakuwa na matukio mbalimbali ya kijamii kama kuchangia damu, kufanya usafi, kutembelea na kusaidia wagonjwa na watu wenye uhitaji
Lakini pia wiki ya Simba ya mwaka huu itatumika kuwakumbuka wakongwe waliowahi kucheza Simba zamani kwa kuwatembelea na kuzindua Matawi ya klabu
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Zambia, Power Dynamo wamealikwa SIMBA DAY ambapo watacheza na Simba katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Aidha Mtendaji Mkuu wa Simba Imani Kajula amesema siku ya Simba Day kibegi cha Simba kitapigwa mnada pamoja na jezi zake na mapato yatakwenda kusaidia kinamama Hospitali ya Muhimbili na Zanzibar
Benki ya CRDB itashirikiana na Simba katika kipindi chote cha wiki ya Simba pamoja na siku ya kilele August 06



