Droo ya hatua za awali ligi ya mabingwa imefanyika Misri leo
Yanga mabingwa wa Tanzania Bara wataanzia hatua ya awali wakati watani zao Simba watakaoshiriki African Football League wataanzia raundi ya kwanza
Hatua ya awali Yanga itaanzia ugenini dhidi ya Asas Fc ya Djibout na kama itafanikiwa kuvuka, raundi ya kwanza itachuana na mshindi kati ya Fc Otoho (Congo) dhidi ya Al Marrikh (Sudan)
Simba itasubiri mshindi wa mchezo kati ya African Star (Namibia) dhidi ya Power Dynamos ya Zambia
Aidha Simba inaweza kucheza mechi tatu na Dynamos kama Wazambia hao watafanikiwa kuvuka hatua ya awali
Simba na Power Dynamos zitachuana kwenye mchezo wa SIMBA DAY August 06



