Droo Ligi ya Mabingwa yafanyika Misri

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th July 2023


Droo Ligi ya Mabingwa yafanyika Misri

Droo ya hatua za awali ligi ya mabingwa imefanyika Misri leo

Yanga mabingwa wa Tanzania Bara wataanzia hatua ya awali wakati watani zao Simba watakaoshiriki African Football League wataanzia raundi ya kwanza

Hatua ya awali Yanga itaanzia ugenini dhidi ya Asas Fc ya Djibout na kama itafanikiwa kuvuka, raundi ya kwanza itachuana na mshindi kati ya Fc Otoho (Congo) dhidi ya Al Marrikh (Sudan)

Simba itasubiri mshindi wa mchezo kati ya African Star (Namibia) dhidi ya Power Dynamos ya Zambia

Aidha Simba inaweza kucheza mechi tatu na Dynamos kama Wazambia hao watafanikiwa kuvuka hatua ya awali

Simba na Power Dynamos zitachuana kwenye mchezo wa SIMBA DAY August 06 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.