Klabu ya Singida Fountain Gate imetangaza Agosti 2, 2023 kuwa ni siku ya tamasha lao la Singida Big Day litakalofanyika uwanja wa Liti mjini Singida
Kupitia tamasha hilo, Singida FG itatambulisha kikosi chake chote kitakachotumika msimu wa 2023/24 pamoja na kucheza mechi ya kirafiki
Huu utakuwa msimu wa pili kwa Singida FG kuandaa Tamasha kama hilo wakifanya mwaka uliopita pia
Kikosi cha Singida FG kimeweka kambi mkoani Arusha kujiandaa na Tamasha hilo pamoja na mchezo wa nusu fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Simba utakaopigwa August 10 katika uwanja wa Mkwakwani



