Yanga - Local

Yanga yataka makundi Ligi ya Mabingwa

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
26 Jul 2023
Yanga yataka makundi Ligi ya Mabingwa

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema malengo ya chini katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika inayotarajiwa kuanza mwezi ujao ni kutinga hatua ya makundi

Katika droo ya mechi za awali na raundi ya kwanza ambayo ilifanyika jana huko Misri, Yanga imepangwa kuanzia Djibout kuikabili Asas Fc

Mechi ya mkondo wa kwanza itapigwa kati ya August 15-20 na mechi ya marudiano itapigwa wiki moja baadae jijini Dar es salaam

Kama Yanga itafanikiwa kufuzu hatua ya awali kwenye raundi ya kwanza itacheza dhidi ya mshindi wa mechi kati ya Otoho Fc ya Congo dhidi ya Al Marreikh ya Sudan

Katika raundi ya kwanza pia Yanga itaanzia ugenini na kumalizia mechi ya pili nyumbani

Kamwe amesema wanajiandaa kwa mechi hizo na jambo muhimu ni kuwaheshimu wapinzani wao

"Sisi kama Yanga Africans tumeipokea vizuri droo iliyopangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika. Nataka niwaambie Wanachama na mashabiki wetu kuwa hakuna timu ndogo kwenye Ligi ya Mabingwa, kila timu inajiandaa ili kuweza kufanya vizuri"

"Tuna muda mrefu sana hatujacheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika. Msimu uliopita ulikuwa mzuri kwetu tukifanikiwa kucheza fainali ya kombe la Shirikisho la CAF. Msimu huu malengo ya klabu ni kuona kwanza tunatinga hatua ya makundi"

"Nawaomba Wanachama na Mashabiki wetu tuhamishe nguvu zetu kwenye michuano hii, tuhakikishe tunacheza hatua ya makundi," alisema Kamwe

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
14m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
29m ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
1h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
2h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
14h ago
READ MORE →