Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Julai 27 2023

Joel JJ By Joel JJ • 27th July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Julai 27 2023

Manchester United wametoa ofa ya mdomo ya euro 50m sawa na £42.8m pamoja na euro 10m (£8.5m) kama nyongeza kwenda Atalanta kwa ajili ya mshambuliaji wa Denmark Rasmus Hojlund, 20. (Athletic)

Mkurugenzi wa michezo wa Juventus Cristiano Giuntoli atasafiri kwenda Uingereza kufanya mazungumzo ya mkataba wa mkopo na klabu ya Chelsea kwa ajili ya mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 30. (Calciomercato, via Goal)

Lukaku yuko jijini London wakati wachezaji wengine wa The Blues wapo kwenye ziara ya kujiandaa na msimu mpya nchini Marekani. (Times) Mshambuliaji wa Ufaransa na Paris St-Germain Kylian Mbappe, 24, hataki kukutana na wawakilishi wa Al-Hilal kuhusu uwezekano wa kuhamia Saudi Arabia. (Sky Sports)

Vyanzo vilivyo karibu na mazungumzo hayo vinazidi kushawishika kwamba Mbappe amekubali masharti ya kujiunga na Real Madrid mwakani. (Telegraph)

Chelsea wanaonekana kushindwa kumpata kiungo wa kati wa Argentina Paulo Dybala, kwa kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 ameripotiwa kusaini mkataba mpya kusalia Roma. (Tuttomercatoweb)

West Ham wanaweza kukosa kumsajili kiungo wa kati wa England Conor Gallagher, 23, ambaye anataka kusalia Chelsea na kupigania namba katika kikosi cha kwanza chini ya bosi mpya Mauricio Pochettino. (Mail)

Al-Hilal wako katika hatua za mwisho katika jitihada zao za kumsajili kiungo wa kati wa Paris St-Germain na Italia Marco Verratti, 30. (Fabrizio Romano).

Wakati huohuo, The Hammers wanaendelea na mazungumzo na kiungo wa kati wa Southampton na England James Ward-Prowse, 28, hikiaminika sasa kwamba makubaliano yanawezekana kufikiwa. (Football Insider)

Liverpool wako tayari kuboresha dau lao la awali la pauni milioni 37 ili kumnunua kiungo wa kati wa Southampton na Ubelgiji Romeo Lavia, 19. (Athletic)

Vilabu hivyo viwili vimetofautiana kuhusu thamani ya kinda huyo, Lavia, kwa tofauti ya takriban £15m. (Telegraph)

Wekundu hao wa Anfield pia wanatarajiwa kukubali ofa ya pauni milioni 40 kutoka klabu ya Al-Ittihad ya Saud Arabia kwa ajili ya kiungo wa kati wa Brazil Fabinho, 29, baada ya mazungumzo kuanza upya wiki hii. (Times)

Kiungo wa kati wa PSG na Ureno Renato Sanches, 25, anakaribia kusaini mkataba wa mkopo kuchezea klabu ya Serie A ya Roma kwa msimu mzima. (L'Equipe)

Matumaini ya Aston Villa kumsajili kiungo wa kati wa Tottenham na Argentina Giovani Lo Celso yameongezeka kwakuwa Napoli ambayo ndio chaguo lake la kwanza bado haijamalizana na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Birmingham Live)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.