Mchezo wa nne wa kirafiki ambao Azam Fc walicheza jana dhidi ya Stade Tunisien ulivunjika dakika ya 60 baada ya Azam Fc kutoridhishwa na maamuzi wa mchezo huo
Mpaka mchezo unavunjika, Azam Fc walikuwa nyuma kwa mabao 3-1
Msemaji wa Azam Fc Hasheem Ibwe amesema mwamuzi alikuwa na upendeleo wa wazi lakini pia wapinzani wao hawakuchukulia mchezo huo kama wa kirafiki
"Mwamuzi alifanya upendeleo wa dhahiri pia hakuchukua hatua kwenye matukio ya rafu ambayo wachezaji wetu walifanyiwa. Dakika ya 60 mchezo ulivunjika baada ya mchezaji wetu Edward Charles Manyama kufanyiwa madhambi ambayo yalipelekea akavunjika mkono"
"Lakini pia mwamuzi akawapa wapinzani wetu mkwaju wa penati, maamuzi ambayo yalipelekea kocha kuagiza wachezaji watoke uwanjani na mchezo huo kuvunjika," alisema Ibwe
Katika mechi za kirafiki ambazo Azam Fc wamechezaji huko Tunisia, walishinda mechi mbili na kupoteza mechi mbili



