Manyama nje wiki moja

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th July 2023


Manyama nje wiki moja

Beki wa Azam Fc Edward Charles Manyama ambaye aliumia katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Stade Tunisien anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu

Manyama aliumia mkono katika mchezo ambao haukumalizika kwa kile kilichoelezwa na Azam Fc kuwa ulitawaliwa na matukio ya vurugu

Taarifa ya Azam Fc imebainisha kuwa Manyama atakuwa nje ya uwanja wa kwa muda wa wiki moja

"Beki wetu Manyama aliyepata majeraha kwenye mchezo siku ya Jumatano dhidi ya Stade Tunisien, anaendelea vizuri hivi sasa. Tofauti na matarajio ya awali tukidhania amevunjika mkono, mara baada ya kupelekwa hospitali na kufanyiwa vipimo kwa kina, imebainika ameteguka mkono wake wa kushoto"

"Daktari wa timu yetu, Dk. Mwanandi Mwankemwa, ameweka wazi kuwa Manyama atakaa nje ya dimba kwa muda wa wiki moja kabla ya kuruhusiwa kurejea kwenye mazoezi ya kawaida na wenzake," ilisema taarifa ya Azam Fc


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.