Beki wa Azam Fc Edward Charles Manyama ambaye aliumia katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Stade Tunisien anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu
Manyama aliumia mkono katika mchezo ambao haukumalizika kwa kile kilichoelezwa na Azam Fc kuwa ulitawaliwa na matukio ya vurugu
Taarifa ya Azam Fc imebainisha kuwa Manyama atakuwa nje ya uwanja wa kwa muda wa wiki moja
"Beki wetu Manyama aliyepata majeraha kwenye mchezo siku ya Jumatano dhidi ya Stade Tunisien, anaendelea vizuri hivi sasa. Tofauti na matarajio ya awali tukidhania amevunjika mkono, mara baada ya kupelekwa hospitali na kufanyiwa vipimo kwa kina, imebainika ameteguka mkono wake wa kushoto"
"Daktari wa timu yetu, Dk. Mwanandi Mwankemwa, ameweka wazi kuwa Manyama atakaa nje ya dimba kwa muda wa wiki moja kabla ya kuruhusiwa kurejea kwenye mazoezi ya kawaida na wenzake," ilisema taarifa ya Azam Fc



