Uhamisho wa wachezaji katika klabu ya Chelsea unakaribia kukamilika na klabu sasa inalenga kuleta vipaji vipya
Baada ya mkutano na mmiliki Todd Boehly, kocha Mauricio Pochettino na mkuu wa uajiri, walipitisha usajili wa kiungo Moises Caicedo wa Brighton
Brighton wanamthaminisha Caicedo kwa pauni 80m na Chelsea wako tayari kulipa kiasi hicho cha fedha. Caicedo amekubali masharti binafsi lakini mkataba bado haujasainiwa
Aidha Mshambuliaji wa kuchukua nafasi ya Christian Pulisic pia yuko kwenye ajenda na imeelezwa kwamba kufuatia ofa ya awali ya Β£20m, ambayo imekataliwa, mkutano mwingine na klabu ya Ufaransa Montpellier unapangwa kwa ajili ya Elye Wahi
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 atapelekwa kwa mkopo Strasbourg kwa miezi michache
Kiungo mshambuliaji wa Ajax, Mghana Mohamed Kudus pia yuko katika hesabu huku vyanzo mbalimbali vinathibitisha kuwa ofa ya kumnunua kiungo mshambuliaji na winga Michael Olise imetumwa kwa Crystal Palace
Wachezaji wawili wapya waliosajiliwa na Chelsea tayari wamemvutia Pochettino kwenye ziara ya majira ya kiangazi ya The Blues walipoilaza Brighton 4-3. Nicolas Jackson alifunga bao lake la kwanza na Christopher Nkunku pia amefunga mabao mawili katika michezo miwili