Bayern kuongeza dau kumnasa Kane

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th July 2023


Bayern kuongeza dau kumnasa Kane

Kwa mujibu wa talkSPORTS, Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy anatazamiwa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wa Bayern Munich kuhusu mustakabali wa Harry Kane leo

Bayern walikuwa na ofa ya pauni milioni 70 kwa nahodha huyo wa Uingereza iliyokataliwa mapema mwezi huu lakini wako tayari kuboresha dau hilo

Washauri wa Kane wameonyesha kuwa yuko tayari kujiunga na mabingwa hao wa Bundesliga

Mshambulizi huyo, ambaye leo anatimiza miaka 30, ameingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake Tottenham

Levy anamthamini Kane kwa pauni milioni 100 na inafikiriwa kuwa Bayern wako tayari kulipa hadi pauni milioni 86

Miamba hao wa Ujerumani wanaweza kusubiri kufikia makubaliano ya awali ya mkataba na Kane mwezi Januari kabla ya uhamisho wa bure, ingawa wanaweza kukabiliwa na ushindani mkubwa.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.