Kwa mujibu wa talkSPORTS, Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy anatazamiwa kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wa Bayern Munich kuhusu mustakabali wa Harry Kane leo
Bayern walikuwa na ofa ya pauni milioni 70 kwa nahodha huyo wa Uingereza iliyokataliwa mapema mwezi huu lakini wako tayari kuboresha dau hilo
Washauri wa Kane wameonyesha kuwa yuko tayari kujiunga na mabingwa hao wa Bundesliga
Mshambulizi huyo, ambaye leo anatimiza miaka 30, ameingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake Tottenham
Levy anamthamini Kane kwa pauni milioni 100 na inafikiriwa kuwa Bayern wako tayari kulipa hadi pauni milioni 86
Miamba hao wa Ujerumani wanaweza kusubiri kufikia makubaliano ya awali ya mkataba na Kane mwezi Januari kabla ya uhamisho wa bure, ingawa wanaweza kukabiliwa na ushindani mkubwa.



