Manchester City - International

Mahrez afuata mamilioni Saudia

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jul 2023
Mahrez afuata mamilioni Saudia

Riyad Mahrez amekamilisha uhamisho wake wa pauni milioni 30 kutoka Manchester City kwenda klabu ya Saudia Al Ahli - na sasa atalipwa pauni 750,000 kwa wiki kwa miaka miwili 

City wamethibitisha kuwa dili hilo limetimia baada ya Al Ahli kufikia bei waliyoomba kwa winga huyo wa Algeria, ambaye alishinda mataji manne ya Ligi Kuu, mawili ya FA, matatu ya Carabao Cup na Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati alipokuwa Etihad baada ya kujiunga na klabu hiyo kwa mara ya kwanza kwa Mkataba wa £60m kutoka kwa Leicester miaka mitano iliyopita

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 aliamua kutimkia Saudia baada ya Pep Guardiola kumuacha nje ya timu yake kwa fainali ya Kombe la FA na fainali ya Ligi ya Mabingwa huku The Blues wakishinda mara tatu msimu uliopita

Mahrez, ambaye pia alishinda Ligi ya Premia akiwa na Leicester, amesisitiza kwamba anaondoka bila majuto

"Kuichezea Manchester City imekuwa heshima na fursa. Nilikuja City kushinda mataji na kufurahia soka langu na nilifanikisha hayo yote na mengine mengi. Nimekuwa na miaka mitano isiyoweza kusahaulika na klabu hii ya soka, nikifanya kazi na wachezaji bora, mashabiki bora na meneja bora zaidi duniani"

"Nimejiwekea kumbukumbu nzuri maishani na namna tulivyoshinda taji la Ligi Kuu ya England na vita ambavyo tumekuwa navyo na Liverpool na, mwaka jana, Arsenal, ilisisitiza hamu na mawazo yetu ya kuwa bora zaidi. Manchester City daima itakuwa sehemu kubwa na yenye furaha maishani mwangu," alisema

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’