Simba - Local

Simba yasisitiza, Simba Day ni kwa Mkapa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jul 2023
Simba yasisitiza, Simba Day ni kwa Mkapa

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amewataka mashabiki waendelee kununua tiketi kuelekea SIMBA DAY ambayo itafanyika August 06 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Ahmed amewahakikishia Wanasimba kuwa Tamasha hilo litafanyika uwanja wa Benjamin Mkapa kama lilivyopangwa, maboresho ya uwanja huo hayaingiliani na ratiba ya Tamasha hilo kubwa zaidi la michezo nchini

"Baada jana kutangazwa ukarabati wa Uwanja wa Benjamini Mkapa, wengi wamekuwa na hofu juu mustakabali wa Tamasha letu la Simba Day"

"Taarifa rasmi ni kwamba hakuna mabadiliko ya Uwanja, Simba Day yetu itafanyika pale pale nyumbani kwetu Benjamini Mkapa"

"Muhimu mashabiki endeleeni kununua tiketi," aliandika Ahmed katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii

Katika hatua nyingine, Ahmed amesema bado mpinzani ambaye atacheza na Simba kwenye SIMBA DAY ni Mabingwa wa Ligi Kuu ya Zambia, Power Dynamo licha ya uwezekano wa Simba kukutana na Dynamo kwenye raundi ya kwanza ligi ya mabingwa barani Afrika

"Mpaka sasa bado hakuna mabadiliko, mpinzani tutakaecheza nae kwenye SIMBA DAY ni Power Dynamo. Tunafahamu upo uwezekano wa kukutana nao kwenye ligi ya mabingwa, kwa upande mwingine hii inafikirisha kidogo kwa sababu tunaweza tukacheza nao mara tatu"

"Lakini Simba ina viongozi makini ambao wanajua vyema kazi yao, kama wataona kuna ulazima wa kubadili mpinzani kwa muktadha wa kiufundi basi watatuambia ingawa kwa muda uliobaki sioni kama hilo litatokea"

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’