Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Julai 29 2023

Joel JJ By Joel JJ • 29th July 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Julai 29 2023

Bayern Munich wameanza mazungumzo na Brentford kuhusu mpango wa kumnunua kipa wao Mhispania David Raya, 27, huku mlinda mlango wa mabingwa hao wa Uswizi Yann Sommer, 34, akijadili kuhamia Inter Milan. (Sky Sports)

Bayern pia wamekubali ombi la Al-Nassr kumnunua mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane, 31. (Fabrizio Romano)

Wakuu wa Bayern hawatasafiri kwenda London kukutana na wawakilishi wa Tottenham kuhusu mpango wa kumnunua mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 30, lakini klabu hiyo ya Ujerumani bado inawasiliana na Spurs. (Sky Sports)

Spurs watatumia mazungumzo yao na Bayern kuhusu Harry Kane kujadili nia yao ya kumnunua mshambuliaji wa klabu ya Ujerumani mwenye umri wa miaka 18 Mathys Tel. (Telegraph - usajili unahitajika)

Chelsea wamekataa ombi la Juventus la kutaka kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 30, kwa sababu wanataka kumuuza kabisa. (Tuttosport, kwa Kiitaliano)

Paris St-Germain wanakaribia kukamilisha dili la kushtukiza kumsajili winga wa Ufaransa Ousmane Dembele kutoka Barcelona. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ana kifungu cha kutolewa cha £42.8m ambacho kinamalizika Jumatatu. (ESPN)

Newcastle United imemuuza winga Mfaransa Allan Saint-Maximin, 26, kwa Al-Ahli ya Saudi Pro League kwa £30m. (Mail)

Manchester United wako tayari kumruhusu mlinda mlango wa Uingereza Dean Henderson, 26, ajiunge na Nottingham Forest kwa mkopo ikiwa na jukumu la kununua - mradi tu wapate ada hiyo ifikapo Januari. (Manchester Evening News)

Aston Villa haitamsajili winga wa Sporting Lisbon na Ureno Pedro Goncalves, 25, kwa sababu ofa yao ya juu ya £38.6m ilikuwa pauni milioni 30 pungufu ya bei ya Sporting. (Recorg, kwa Kireno)

Galatasaray wanavutiwa na kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Fred, 30, lakini kuna pengo katika uthamini kati ya klabu hizo mbili. (Sky Sports)

Nottingham Forest imekataa ombi la rekodi ya klabu la £35m kutoka kwa Brentford kwa ajili ya mshambuliaji wao wa Wales Brennan Johnson, 22. (Telegraph - usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.