Azam imedhamiria ubingwa Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th July 2023


Azam imedhamiria ubingwa Ligi Kuu

Azam Fc imefanikiwa kun'goa silaha mbili muhimu kutoka klabu ya Yanga ili kukiimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao

Walianza na Feisal Salum 'Fei Toto', mchana wa leo wakatangaza kuinasa saini ya mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC msimu 2021/22, Yannick Bangala kutoka klabu ya Yanga

Fei Toto na Bangala walikuwa wachezaji muhimu katika kikosi cha aliyekuwa kocha wa Yanga Nasreddine Nabi

Kwa aina ya usajili ambao Azam Fc wamefanya, wameonyesha kwa vitendo kuwa wanataka kushindana na Yanga na Simba katika soka la Tanzania

Pengine huenda wakafanikiwa katika huu msimu unaokuja


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.