Azam Fc imefanikiwa kun'goa silaha mbili muhimu kutoka klabu ya Yanga ili kukiimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao
Walianza na Feisal Salum 'Fei Toto', mchana wa leo wakatangaza kuinasa saini ya mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC msimu 2021/22, Yannick Bangala kutoka klabu ya Yanga
Fei Toto na Bangala walikuwa wachezaji muhimu katika kikosi cha aliyekuwa kocha wa Yanga Nasreddine Nabi
Kwa aina ya usajili ambao Azam Fc wamefanya, wameonyesha kwa vitendo kuwa wanataka kushindana na Yanga na Simba katika soka la Tanzania
Pengine huenda wakafanikiwa katika huu msimu unaokuja



